1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Macron kufanya ziara rasmi Ujerumani Mei 26

2 Mei 2024

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anatarajiwa kufanya ziara rasmi nchini Ujerumani mwishoni mwa mwezi Mei, baada ya kufutwa kwa safari yake ya mwezi Julai mwaka jana.

https://p.dw.com/p/4fRL3
Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron
Rais wa Ufaransa Emmanuel akiwa na Kansela wa Ujerumani laf ScholzPicha: Ebrahim Noroozi/AP/picture alliance

Safari ya Macron ilifutwa kutokana na maandamano makubwa yaliyoshuhudiwa nchini Ufaransa kufuatia mauaji ya kijana Nahel.

Macron na mkewe Brigitte wanatarajiwa kuwasili Berlin Mei 26 na watapokelewa kwa heshima zote za kiitifaki katika Ikulu ya Bellevue na Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier na mkewe Elke Büdenbender.

Soma pia:Macron: Ulinzi wa Ulaya unapaswa kuwa zaidi ya NATO

Hii itakuwa ziara ya kwanza ya kiserikali kufanywa na rais wa Ufaransa tangu ile iliyofanywa na hayati Jacques Chirac mnamo mwaka 2000.

Mjini Berlin, Macron atahudhuria tamasha litakalofanyika kwenye Bunge la Ujerumani Bundestag kuashiria maadhimisho ya miaka 75 ya katiba ya nchi hii.