1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Bunge la Vietnam laidhinisha uamuzi wa Spika kujiuzulu

2 Mei 2024

Bunge la Vietnam limeidhinisha uamuzi wa Spika wa Bunge Vuong Dinh Hue kujiuzulu, huku Chama tawala cha Kikomunisti kikiendesha operesheni kali dhidi ya ufisadi.

https://p.dw.com/p/4fRKF
Spika wa Bunge Vuong Dinh Hue
Aliekuwa Spika wa Bunge Vuong Dinh HuePicha: Nhac Nguyen/AFP/Getty Images

Hatua ya kuondoka kwa Hue ambayo ilitangazwa tangu wiki iliyopita na Kamati kuu ya Chama, inaiacha Vietnam katika ombwe la uongozi baada ya rais Vo Van Thuong kujiuzulu mwezi Machi, na hivyo kuacha nafasi mbili za juu kati nne bila uongozi.

Soma pia:Ziara ya Xi Vietnam kunatishia usahwishi wa Marekani?

Mnamo Mei 20, Bunge la Vietnam limepanga kuanza mkutano utakaodumu kwa mwezi mzima na ambao unatarajiwa kumteua rais na Spika mpya wa bunge baada ya watu hao kuteuliwa na chama cha Kikomunisti.